Skip to main content

IJUE TECHNOLOGIA YA HABARI

TUMIA MITANDAO YA KIJAMII KUJITENGENEZEA FURSA ZA MAENDELEO.



Mwaka 2011,nilipata kufuatilia kwa ukaribu kuhusu mitandao ya kijamii.Nilipata muda wa kuchambua mtandao mmoja baada ya mwingine,nilipaswa kufanya hivyo ili kubaini ni nani ni gwiji kati ya mitandao hiyo.Nilipata kujua tofauti kati ya mtandao mmoja na mwingine,na kwanini mtu utumie mtandao huu na usitumie mwingine.Na mwisho wa siku nilikuja kutambua ya kwamba Facebook ndiyo ulikuwa mtandao uliotengenezwa kwa ubunifu wa hali ya juu,na unaotoa huduma nyingi zaidi ukifana nisha na mitadano mingine,kama twitter, linked in ,my space na mitandao mingineyo.Uchunguzi huo ulinichukua muda,takribani mwezi mmoja.

Matumizi ya mitandao ya kijamii imebadili maisha ya watu wengi sana,haswa namna ya upashanaji habari.Taarifa zimekuwa zikiwafikia watu wengi sana ndani ya muda mfupi,na vyanzo vya habari vimeongezeka,ukilinganisha na miaka ya nyuma,na hii ni changamoto kwa TCRA katika kudhibiti ubora na ukweli wa habari zinazowafikia mamia ya watu.
Kuongezeka kwa watumiaji wa mitandao ya kijamii,ni ishara tosha ya kwamba watanzania walio na uelewa juu ya matumizi ya internet unaongezeka,ni jambo jema hilo,ingawa tunapaswa kujiuliza maswali ya msingi,je watumiaji wa internet wanatumia kwa usahihi,na je tunatumia viwango(standards) vipi kuamua ya kwamba mtu huyu anatumia kwa usahihi na huyu hatumii kwa usahihi.Hayo yote tunapaswa kutafakari na kuchukua hatua.
Watumiaji wengi wa mitandao ya kijamii ni vijana na wengi wao hutumia mitandao ya kijamii kwa ajili ya kuchart,kupost picha ambazo hazina mantiki na nyingi ni picha ambazo zimekosa maadali. kitu ambacho kinawapotezea muda mwingi,na kuharibu fikra zao na kupunguza uwezo wao wa kujikita katika masuala ya msingi,matokeo yake tumekuwa na vijana wengi ambao hawajikita katika kujiletea maendeleo yao binafsi. Kuna fursa nyingi sana kwenye mitandao ya kijamii,iwapo tu mtumiaji ataamua kutumia mitandao ya kijamii kama sehemu ya kujitengenezea fursa.
Na ni wito wangu kwa vijana kutumia mitandao ya kijamii kwa ajili ya kujitengenezea fursa za maendeleo yao.Tusipoteze muda kwenye masuala ambayo si ya msingi pindi tunapokuwa internert bali tutumie muda wetu kwenye kujifunza na kudadisi masuala ya msingi yanayoweza kutufanya tuanze kujiletea maendeleo.

 Makala hii imeandikwa
na Baraka Daniel Kiranga(24)
"ni makala nzuri ambayo Baraka danielkiranga alifikiria sana unaweza ona matumizi ya mitandao yanavyoonekana kitofauti kwa wachache mpaka ikasababisha watumiaji wengine kuichukia mitandao hiyoikisoma kwamakiniutaona  mitandao inafaida sana katika jamii ikitumika vizuri"

Comments

Popular posts from this blog

5 Steps To Get Your Voice Heard At Meetings

Follow these five steps to get your voice heard during your next meeting. Master the pre-meeting Before the meeting, find something on agenda that you are passionate about and prepare a statement that expresses a strong opinion or idea that goes beyond agreeing with the status quo. “Women tend to speak in meetings when they agree with something that is already on the floor,” Adams says. “Work on putting a new idea out there first.” Arrive before the meeting starts and make small talk as colleagues come in, she says. This allows you to get comfortable with your voice in the room without any high stakes. “You are more apt to speak up during a meeting if you’ve already spoken to people,” she says. Use power language Get to the point and be clear about what you want. For instance, Adams says, there is a big difference between saying “I want this project to be successful so here’s what we should do” versus “Let’s take another look at this.”  Banish qualifying wor...

IJUE TECHNOLOGIA YA HABARI

Karibuni katika blog yangu kujifunza na kuelewa umuhimu wa habari katika jamii inayotuzunguka.......... katika jamii inayotuzunguka technologia ya habari imekua tofauti na kile ambacho kinadhaniwa katika jamii. inajulikana kama ni technologia iliyo na mitazamo hasi katika jamii kwa mfano mitandao ya jamii imekua ikiangaliwa katika mitazamo hasi katika jamii maana imekua ikipotosha jamii. HIVYO VYOTE VIMEBEBWA NA TECHNOLOGIA YA HABARI hiyo ni mitazamo ya baadhi na wanajamii wasio kua na uelewa wa hii technologia ya habari. leo nataka nikufungue na nikueleze maana na matumizi ya hii technologia ya habari katika jamii ya leo....... Nafurahi kuwa utanielewa na maana  Technologia ya habari inahusika na matumizi ya kompyuta zitumiazo umeme na programu za kompyuta kubadili, kuhifadhi, kulinda, kuchecheta, kueneza, na usalama katika kupokea habari. Hiyo ndo maana ya technologia ya habari na siyo kama wanajamii baadhi wanavyo ielewa. endelea kuwa na mimi katika kuji...

maonyesho ya kiteknolojia duniani

Kwa zaidi ya siku tatu  nimekua nikifuatilia maonyesho ya kiteknologia inchini Barcelona Hispania ambapo makampuni mbalimbali na makubwa ya dunia yamekusanyika kuonyesha ukali wao kwenye maswala ya digital. Mpaka sasa HUAWEI wameendelea kuongoza kwa kuzimiliki headlines kubwa za dunia kutokana na bidhaa mbalimbali walizozindua ambapo leo ilikua ni zamu ya hii saa ya kisasa. Ni saa ambayo pamoja na mambo mengine, inakupa muda kama zilivyosaa nyingine, simu yako inaweza kuwa mbali na wewe lakini hii saa ikakuonyesha nani anakupigia, inakupa utabiri wa hali ya hewa, kuna sehemu ya kukutunzia kumbukumbu za vitu unavyotaka kufanya. Kingine kikubwa nilichopenda ni kwamba ina uwezo wa kukutelea taarifa mpya kila wakati kama umepata msg Facebook, kwenye email na mitandao mingine ya kijamii. Hizo ni baadhi ya sifa zake tu. Inapatikana katika muonekano tofauti kama inavyoonekana hapa. Unaweza kutazama video ya maelezo mengine ya hii saa kwa ku...